Na Mwandishi
wetu
Chama cha
Wadau wa Nishati Jadidifu (TAREA) kimewahimiza wananchi kuwa makini dhidi ya
watu wanaowauzia vifaa vya umeme jua mtaani wakidai kuwa ni promosheni kwa vile
vingi vimebainika kuwa ni feki.
Agizo hilo
linafuatia baada ya wananchi wa mikoa ya Kilimanjaro, Manyara na Arusha kulizwa hasa baada kuuziwa vifaa
vinavyojulikana kama solar panel na baadaye kugundua kuwa havifanyi kazi.
Akizungumza
na blogu hii jijini Dar es Salaam Katibu Mtendaji wa Tarea Injinia Mathew
Matimbwi alisema katika kijiji cha Magadini na Simanjiro wananchi waliuziwa
vifaa hivyo na mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la moja la Bernad na
kuwaeleza kuwa wachaji masaa 8 kisha watumie lakini walivyofanya hivyo
havikufanya kazi.
Alisema
mfanyabiashara huyo alitoa namba ya simu hii 0759953583 akidai anatoka katika
kampuni ya vifaa hivyo inayoitwa SOLAR AFRIQUE akidai Ofisi zake zipo Ubungo
Plaza Dar es Salaam na Mwanza.
“Jambo la
ajabu mfanyabiashara huyo akipigiwa simu hapokei inaita tu na kukata na namba
za simu za kampuni zinazoonekana kwenye risiti ambazo amekuwa akizitoa pia
hazipokelewi,” alisema Injinia Matimbwi.
Alisema
wananchi hao baada ya kuona vifaa havifanyi kazi walimpa risiti na vile vifaa
Mwalimu mmoja anayefahamika kwa jina la Emmanuel Madauda ambaye alikuwa na
safari za kuja Dar es Salaam ndipo wale wananchi wakamwomba aje navyo kwenye
kampuni hiyo ambayo imeandikwa kwamba iko Dar es Saalam na Mwanza.
Hata hivyo,
baada ya Mwalimu huyo kufuatilia pale Ubungo Plaza alielezwa hakuna Kampuni
kama hiyo na hivyo kupewa orodha na kampuni zilizoko pale na ndipo kuelekezwa
akaulizie TAREA ili wamsaidie.
Mwalimu huyo
alibeba risiti mbili zenye majina ya wananchi waliouziwa vifaa hivyo feki kama ushahidi ili aje kuulizia kwenye
kampunii hiyo ikiwezekana warudishe fedha zao.
Kwa mujibu
wa Mwalimu Madauda alisema Bernad ambaye ndiye mfanyabiashara huhisiwa kwamba ni raia
wa Kenya kutokana na lafudhi ambayo alikuwa akiongea ila amekuwa akiuza bidhaa
hizo nchini kwa madai kuwa ni za hapa nchini wakati hiyo Kampuni haipo.
Matimbwe
alisema mbaya zaidi vifaa hivyo wananchi wa mikoa hiyo wamekuwa wakiuziwa kwa
bei ya shilingi 40,000 wakielezwa ni bei ya promosheni lakini ukweli haviuzwi
kwa bei hiyo wala haviuzwi kimoja kimoja kama ambavyo wananchi wameuziwa.
Alisema
kutokana na tukio hilo wananchi wanatakiwa kujifunza kutokana na makosa na kwamba
watazungumza na tume ya ushindani ili kushughulia tatizo hilo ili ikiwezekana
wahusika wachukuliwe hatua kwa kuuza bidhaa feki.
No comments:
Post a Comment