Na Juma
Mohammed,MAELEZO Zanzibar
WIZARA ya Ardhi, Makaazi, Maji na
Nishati Zanzibar imesema lengo la serikali ni kuwafikishia huduma za maji
wananchi wote wa Unguja na Pemba.
Naibu waziri wa wizara hiyo Haji Mwadini
Makame aliwaambiwa wajumbe wa baraza la wawakilishi wakati akijibu masuala
katika kikao cha baraza hilo kufuatia suali la msingi lililoulizwa na
Mwakilishi wa Jimbo la Matemwe (CCM) Abdi Mosi Kombo aliyetaka kujua serikali
imejipanga vipi katika suala la kutatua kero ya upatikanaji wa maji.
Naibu waziri huyo alisema serikali
imejipanga vyema katika kuhakikisha wananchi wote wanapata maji kwa wakati
muafaka na kuahidi kwamba meli ya waya na vifaa hivi karibuni itawasili katika
bandari ya dar es salaam.
Awali Kombo alisema tatizo la maji
kwenye jimbo la Matemwe kutokana na kisima kidogo Matemwe ambacho hakina uwezo
wa kupandisha maji na kuwasaidia wananchi wa kijiji hicho na kuhoji ni lini
serikali itawapatia wananchi wake mashine kubwa ili kuweza kupata huduma hiyo.
Akijibu suali hilo naibu huyo
alisema uingiaji wa pampu siku zote unakwenda sambamba na uwezo wa kisima
ulichonacho ambacho hutokezea dharura mafundi huweka pampu ndogo ndogo kwa muda
wa kuhofia kuwakosesha wananchi huduma hiyo muhimu.
Alisema baada ya hapo hurejesha
pampu ambayo inaenda sambamba na uwezo wa kisima kilichopo na kwa sasa tayari
kisima cha kiachange kishawekewa pampu ambayo inakwenda sambamba na uwezo wa
kisima na hivi sasa maji yanapatikana hadi kigomeni.
Akijibu ni sababu zipi zinzofanya
mashine hiyo iunguwe mara kwa mara Naibu alisema “Sababu hasa zinazopelekea
kuungua kwa mashine hizi ni hitilafu za umeme ikiwemo umeme mdogo ‘low voltage’
katika eneo hilo ambapo tayari ZAWA kwa kushirikiana na ZECO inafanya jithada
kulitatua tatizo hilo” alisema.
SOURCE:Swahilivilla
No comments:
Post a Comment