Na Mwantanga Ame
JUMLA ya Wazanzibari 10,578
wamepatiwa vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi baada ya kukamilisha
masharti ya kisheria ya kuweza kupata vitambulisho hivyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Mwinyihaji Makame, aliyasema hayo
jana wakati akisoma hotuba ya bajeti ya Mapato na Matumizi ya Ofisi kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, huko katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi,
Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Waziri Mwinyihaji, alisema ndani
ya kipindi cha mwaka huu wa fedha Wazanzibari 10.578 wamefanyiwa
usajili kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi.
Alisema katika usajili huo jumla
ya vitambulisho vipya 3,923 vilitengenezwa baada viliopo kumaliza muda
wake wa matumizi huku wafanyakazi wa serikali waliopatiwa huduma hiyo
walifikia 10,393.
Alisema hivi sasa Idara hiyo pia
imeshaandaa rasimu kwa ajili ya kuifanyia marekebisho sheria namba 7 ya
2005 ikiwa ni hatua ya kutoa vitambulisho kwa wageni wanaoishi hapa
nchini.
Alisema rasimu hiyo tayari
imeshapitishwa na Baraza la Mapinduzi na hivi sasa inasubiri kufikishwa
katika Baraza la Wawakilishi ili kuweza kuanza kujadiliwa.
Alisema tangu mfumo huo kuanza
kutumika Idara hiyo imeweza kuhakikisha inatimiza masharti ya kimataifa
kwa mara ya sita mfululizo na imeweza kushinda kufikia viwango bora
duniani.
Alisema kwa ujao wa fedha
itaendelea kusajili Wazanzibari 10,500 wanaotimiza masharti ya usajili
na kuwapatia vitambulisho pamoja kutengeza vitambulisho kwa waliomaliza
muda.
Akizungumzia juu ya Idara ya
Usalama Kazini (GSO), Waziri huyo alisema jumla ya wafanyakazi 554
kutoka katika taasisi mbali mbali za serikali walifanyiwa upekuzi na
taasisi 12 zilikaguliwa kuangalia utunzaji wa siri za seriakali.
Akizungumzia Idara ya
Ushirikiano wa Kimataifa na Uratibu wa shughuli za Wazanzibari Wanaoishi
Nchi Nje, alisema kimeweza kufanya ziara mbali mabali katika nchi za
falme za kiarabu kwa Oman na Dubai ikiwa ni hatua kukutana na
Wazanzibari ili kuwashajiisha katika kushiriki kuchangia maendeleo ya
Zanzibar
Akizungumzia juu ya mradi wa
mageuzi ya Serikali za Mitaa Waziri huyo alisema sera yake imekamilika
baada kupitishwa kwa wadau tofauti zikiwemo taasisi binafsi ikiwa ni
hatua ya kupata maoni yao.
Aidha, upande wa uratibu wa
Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa, Waziri huyo, alisema tayari kuna
mradi ambao utahusisha ujenzi wa misingi ya maji ya mvua kwa ajili ya
maandalizi ya kutafuta mkandarasi ataeifanya kazi hiyo ambayo
inatarajiwa kuyanufaisha maeneo ya ziwa la Sebleni, Ziwa la Mtumwajeni
na Ziwa la kwa binti Amrani.
Maziwa mengine yatayofaidika na
mradi huo Waziri huyo alisema ni la Mantenga, Kwamtipura, Kilima hewa
karakana, Sogea, Mpendae, Jang’ombe, Uwanja wa Demokrasia na Shauri
Moyo.
kwa habari zaidi swahilivilla.blogspot.com
No comments:
Post a Comment