TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Friday 6 July 2012

TAJONET wapitisha rasimu ya katiba

MTANDAO wa Wandishi wa Habari nchini (TAJONET), umefanikiwa kupitisha rasimu ya Katiba ambapo kamati iliyosimamia mchakato wa rasim hiyo, imekabidhiwa  jukumu la kukamilisha usajili ndani ya wiki mbili. 

Mwenyekiti wa Mtandao huo Williamu Shao alisema hayo wakati wa mkutano wa wanachama wakupitia rasimu hiyo ya katiba uliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

 Alisema kupita kwa rasimu hiyo ni mwanzo mzuri hivyo ni wajibu wa kila mwanachama kuisoma na kuielewa vizuri kwa ajili ya utekelezaji wa malengo ya mtandao huo.

 Shao alisema baada ya rasimu hiyo kukubalika kwa wanachama kilichobaki ni kwa wajumbe wa Kamati kuendelea kusimamia zoezi zima la usajili,utakapokamilika mtandao uweze kuamza kazi rasmi.

 “Baada ya kukamilisha usajili wa Katiba yetu wanachama wa  Tajonet watakutana Julai 19, mwaka huu  kwa ajili ya kuangalia jinsi ya kukamilisha  hatua muhimu ya uchaguzi wa kuwapata viongozi watakaohudumu kwa kipindi cha miaka tatu”alisema Shao.

 Aidha, mkutano huo ulipitisha jina la Angela Msangi kuwa Mweka hazina ambapo kwa kauli moja  wamekubaliana kuwa kila mwananachama atawajibika  kuchangia sh. I00,000 ikiwa ni ada ya uwananchama kila mwaka hata hivyo ada hiyo inaruhusiwa kulipwa katika awamu mbili.

 Shao aliwaasa wanachama kuacha kuweka mbele chombo anakotoka na baadala yake kuamini kuwa kila anachofanya ni kwa ajili ya maendeleo na famanikio ya TAJONE kitendo kitakachokamilisha ndoto zao.

 Kwa upande mwingine mtandao huo umetoa shukurani kwa Meneja wa Hoteli ya Break point LT, Daud Machum kwa kujitolea kwake ukumbi bure na sh 20,000 kama kuwaunga mkono katika kile wanachokusudia.

 Naye mweka hazina wa mtandao huo, Angela alisema baada ya wanachama kutakiwa kuchangia mchango wa  papo kwa papo kwa ajili ya kupata fedha za huduma za kikao hicho, zilipatikana zaidi y ash 300,000 kutoka kwa
Wanchama 36 waliodhuria mkutano huo.

 Source:Full Shangwe blog

No comments:

Post a Comment