MTANDAO wa Wandishi wa Habari nchini (TAJONET), umefanikiwa kupitisha
rasimu ya Katiba ambapo kamati iliyosimamia mchakato wa rasim hiyo,
imekabidhiwa jukumu la kukamilisha usajili ndani ya wiki mbili.
Mwenyekiti wa Mtandao huo Williamu Shao alisema hayo wakati wa mkutano
wa wanachama wakupitia rasimu hiyo ya katiba uliyofanyika jijini Dar es Salaam
jana.
Alisema kupita kwa rasimu hiyo ni mwanzo mzuri hivyo ni wajibu wa
kila mwanachama kuisoma na kuielewa vizuri kwa ajili ya utekelezaji wa malengo
ya mtandao huo.
Shao alisema baada ya rasimu hiyo kukubalika kwa wanachama
kilichobaki ni kwa wajumbe wa Kamati kuendelea kusimamia zoezi zima la
usajili,utakapokamilika mtandao uweze kuamza kazi rasmi.
“Baada ya kukamilisha usajili wa Katiba yetu wanachama wa
Tajonet watakutana Julai 19, mwaka huu kwa ajili ya kuangalia jinsi ya
kukamilisha hatua muhimu ya uchaguzi wa kuwapata viongozi watakaohudumu
kwa kipindi cha miaka tatu”alisema Shao.
Aidha, mkutano huo ulipitisha jina la Angela Msangi kuwa Mweka
hazina ambapo kwa kauli moja wamekubaliana kuwa kila mwananachama
atawajibika kuchangia sh. I00,000 ikiwa ni ada ya uwananchama kila mwaka
hata hivyo ada hiyo inaruhusiwa kulipwa katika awamu mbili.
Shao aliwaasa wanachama kuacha kuweka mbele chombo anakotoka na
baadala yake kuamini kuwa kila anachofanya ni kwa ajili ya maendeleo na
famanikio ya TAJONE kitendo kitakachokamilisha ndoto zao.
Kwa upande mwingine mtandao huo umetoa shukurani kwa Meneja wa
Hoteli ya Break point LT, Daud Machum kwa kujitolea kwake ukumbi bure na sh
20,000 kama kuwaunga mkono katika kile wanachokusudia.
Naye mweka hazina wa mtandao huo, Angela alisema baada ya
wanachama kutakiwa kuchangia mchango wa papo kwa papo kwa ajili ya kupata
fedha za huduma za kikao hicho, zilipatikana zaidi y ash 300,000 kutoka kwa
Wanchama 36 waliodhuria mkutano huo.
Source:Full Shangwe blog
No comments:
Post a Comment