Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Peter Kallaghe (wa katikati mwenye suti) akiwa na wawakilishi wa Tanzania wa Michezo ya Olimpiki ya London 2012. [Picha kwa heshima ya Kamati ya Olimpiki ya Tanzania]
Tanzania inapaswa kuchukua mapumziko ya muda
na kusitisha ushiriki wake katika Michezo ya Olimpiki ili kuandaa kwa ufanisi
kizazi kipya kijacho cha wanamichezo, wachambuzi wa michezo wasema.
Katika michezo ya Olimpiki ya London, iliyomalizika Jumapili (tarehe 12 Agosti), wanariadha saba wa Tanzania waliiwakilisha Tanzania, na hakuna hata mmoja aliyeshinda medali. Tanzania imeshinda medali mbili katika mashindano ya Olimpiki, zote huko Moscow mwaka 1980.
Faustine Mussa na
Samson Ramadhani walishiriki katika mbio za marathoni za wanaume lakini
walishindwa kupanda jukwaa la zawadi. Mussa alimaliza nafasi ya 33 alitumia muda
wa saa 2, dakika 17 na sekunde 39, wakati Ramadhani alimaliza wa 66 kwa muda wa
saa 2 dakika 24, sekunde 53. Mwanamarathoni wa tatu, Mohamed Ikoki Msandeki,
alijitoa kwenye mashindano siku moja, kwa kusema alikuwa mgonjwa.
Mkimbiaji wa mbio
za kati Zakia Mrisho alimaliza wa 16 katika mbio za mita 5,000 kwa kutumia muda
wa dakika 15 na sekunde 39.58. Naye mwogeleaji Ammaar Ghadiyali alitokea wa tatu
katika kundi lake na mwogeleaji Magdalena Moshi alitokea wa 7 katika kundi ,
lakini wote walishindwa kuendelea zaidi. Bondia Suleiman Kidunda alipoteza
raundi zote tatu kwenye mashindano ya uzito wa wastani.
Matayarisho mabovu na ukosefu wa uongozi
Mwandishi wa habari za michezo Grace Hoka anasema michezo ya Tanzania inahitaji kugeuzwa kabisa kiasi kwamba serikali ingesitisha ushiriki wa kimataifa katika michezo yote kwa muda wa amiaka 10 ili kukuza michezo ipasavyo nchini na kutoa mafunzo makubwa kwa wanariadha wenye kuleta matumaini.
"Tunapaswa
kuzifumua timu zote za taifa, mashirika yote ya michezo ya taifa na kila kitu
kinachohusiana na michezo na kuanza kuwafunza watoto wadogo. Baada ya miaka 10,
tutakuwa na timu nzuri kuliko wakati wowote," Hoka aliiambia
Sabahi.
Anasema
matayarisho mabovu ya wanariadha na ukosefu wa uongozi kutoka kwa mameneja
katika mashirika ya michezo ndio sababu kubwa ya utendaji wa Tanzania wa kuvunja
moyo katika michezo ya Olimpiki mwaka huu.
Anasema serikali
ingechukua uongozi kutoka mashirika ya michezo, hata kama ni kwa muda, kama
ilivyofanya kwa timu ya taifa ya mpira tangu mwaka 2007.
Zaidi ya hayo,
alisema hata kama itakuwa ghali zaidi, wakimbiaji wa marathoni wanapaswa kufanya
mazoezi huko Arusha au Mbeya, ambako kuna mwinuko wa juu kuliko ilivyo Dar es
Salaam.
Wanamichezo wa
Tanzania wanaonekana wenye akili za kushiriki tu katika michezo ya Olimpiki, na
wala sio kushinda, anasema Cyprian Maro, mkuu wa elimu ya viungo na sayansi ya
michezo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
"Nadhani suluhisho
pekee ni kuzigeuza mashirika ya michezo, kuwapatia mafunzo kizazi kipya na
kurejea kujiunga tena na mashindano ya kimataifa baada ya miaka nane," maro
aliiambia Sabahi.
Maro alisema
serikali imejaribu kuipiga jeki michezo kupitia mabadiliko ya sera.
Mwaka 2008,
serikali ilirejesha michezo katika mtaala wa shule za umma, baada ya
kuusimamisha mwaka 1990. Pia inagharimia programu za maalumu za miaka miwili
katika vyuo 11 kuandaa walimu wa elimu ya viungo na makocha katika shule za
sekondari. Shule za umma huajiri wahitimu kutoka mpango wa mafunzo mara moja
baada ya wao kupata mafunzo ya stashahada.
Hata hivyo, juhudi
hizi hazioneshi kwa mafanikio ya timu kwa sababu mashirika ya michezo, kama vile
Kamati ya Olimpiki ya Tanzania (TOC) na Chama cha Wanariadha cha Tanzania,
hawasimamii vyema mafunzo ya wanamichezo.
Maro alisema
mashirika ya michezo pia yanahitaji kupewa mafunzo ili kuwa na stadi zinazofaa
za uendeshaji.
"Uwezo wa viongozi
wa mashirika ya michezo ni mdogo sana," aliiambia Sabahi. "Wanaweza wakaweka
rekodi za riadha na masumbwi, lakini hii haitoshi. Lazima wawe na uwezo wa
kuandika mapendekezo ya gharama na kupanga michezo, badala ya kungojea
serikali."
Msaada zaidi wa
serikali uhitajika
Katibu Mkuu wa TOC
Juma Ikangaa, mshindi wa medali ya fedha katika marathoni ya Michezo ya Jumuiya
ya Madola mwaka 1982, aliilaumu serikali kwa kutowekeza katika michezo, na
kusema kuwa mengi yanahitajika kufanywa ikiwa Tanzania ina ndoto za
mafanikio.
Alisema serikali
haitoi msaada unaohitajika kwa TOC ili kuwatayarisha wanariadha kwa viwango
vinavyokubalika.
"Hatuwezi kuwa na
programu bila ya pesa. [Kambi za mafunzo zinahitaji] pesa na hizi lazima zitoke
serikalini kama ilivyo kwa nchi nyengine," Ikangaa alisema.
Alisema wafadhili
watakuja mara pale michezo yatakuwa na mafanikio , kwa hivyo serikali inahitaji
kuwekeza mtaji wa awali.
Naibu Waziri wa
Habari, Vijana, Michezo na Utamaduni Amos Makala alielezea majuto ya serikali
kwa utendaji wa wanariadha wa Tanzania katika Olimpiki, lakini aliwahamasisha
Watanzania kucheza michezo zaidi ili kuwa na fursa bora kwenye michezo siku za
usoni.
Bila ya shaka,
matokeo ni mabaya, lakini hatupaswi kuvunjika moyo," Makala aliiambia Sabahi.
"Tujipange wenyewe ili kushiriki katika michezo mingi zaidi kuliko tulivyofanya
mara hii. Tujaribu michezo mengine zaidi ya riadha, kuogelea na
ndondi."
Makala alisema
Tanzania wana vipaji na wanaweza kufanya vizuri zaidi katika michezo ya Olimpiki
ya mwaka 2016 huko Brazili ikiwa watafanya mafunzo na ikiwa TOC itapangwa bora
zaidi.
"Ninawata
Waanzania wawe wabunifu ili kuweza kupata medali zaidi katika michezo ijayo,"
alisema.Source:Swahilivilla Blog
No comments:
Post a Comment