TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Friday 5 October 2012

Mashabiki wa mpira wa miguu Kenya warejea viwanjani

Wapenzi wa mpira wa miguu nchini Kenya wanakwenda kwenye viwanja vya mpira nchini kwa idadi kubwa ili kuangalia timu zao wazipendazo zinazoshindana katika Ligi Kuu ya Kenya (KPL).

 Mashabiki wanajitokeza kwa idadi kubwa mwaka huu kuangalia mechi za Ligi Kuu ya Kenya. [Tony Karumba/AFP]
 
Katika miaka ya karibuni, mahudhurio yamekuwa ya chini huku mechi zikiangaliwa na watu wachache tu. Lakini tangu mwaka jana, ligi imeshuhudia ongezeko la mahudhurio kwa sababu ya kile ambacho wengine wanasema ni kutokana na mipangilio mizuri na ufadhili.
"Nimekuwa nikihudhuria mechi za mpira wa miguu ili kuangalia timu yangu maarufu ya AFC Leopards kwa sababu ligi sasa imeandaliwa vizuri," Oscar Kwena, mwenye umri wa miaka 46, aliiambia Sabahi.
Kwena, mkazi wa Nairobi, alisema kuwa anajua atafaidi thamani ya pesa zake wakati anapokwenda kiwanjani kuangalia timu ake, ambayo kwa sasa ni ya pili katika ligi.
Ligi haiwavutii wanaume tu; wanawake pia wanahudhuria kwa idadi kubwa.
"Ninahakikisha kuwa ninaangalia kila mchezo wakati wowote timu yangu inacheza mechi zake mjini Nairobi," alisema Emily Okindi, msichana mwenye umri wa miaka 22 na mfuasi wa Gor Mahia.
Okindi, mtafutaji kazi anayeishi huko Rongai Rongai, kitongoji nje kidogo ya mji wa Nairobi, aliiambia Sabahi kuwa alianza kuhudhuria mechi za mpira wa miguu mwaka jana. "Hapa ndipo pahali pa kuwepo ikiwa unataka kufaidi burudani kiwanjani na nje ya kiwanja," alisema.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) huko Nairobi Magharibi Simon Mugo aliiambia Sabahi kuwa ligi imepata umaarufu upya kwa sababu ya mpangilio wake mzuri na ufadhili bora zaidi wa timu.
"Ufadhili wa timu tano za juu katika ligi kutoka kwa mashirika kumeipa msukumo. Sasa tuna mechi zinazooneshwa moja kwa moja na DStv," alisema.
Timu za juu zimepata ufadhili kutoka makampuni makubwa. AFC inafadhiliwa na Kampuni ya Sukari ya Mumias, Gor Mahia na Kiwanda cha Maziwa cha Broookside Dairy na Sofapaka inafadhiliwa na Kampuni ya Saruji ya East African Portland.
Tiketi kwa mechi nyingi zinauzwa kwa shilingi 500 (dola 6.2) kwa viti vya VIP na shilingi 200 (dola 2.5) kwa viti vya kawaida. Uwanja wa Nyayo ambako mechi nyingi huchezwa, una uwezo wa kuchukua watu 30,000.
Sehemu ulipo uwanja huo. kilomita tatu kutoka katikati ya mji, na usalama ulioimarika wakati wa mechi, pia kumesaidia ongezeko la mahudhurio mchezoni, Mugo alisema.
"Siku zimepita ambao urushaji mawe ulikua jambo la kawaida katika mechi za mpira wa miguu," Mugo alisema, na kuongeza kuwa FKF inafanya kazi na polisi ili kuimarisha usalama katika viwanja vyote.
Ufadhili bora zaidi pia umepelekea kuwepo na wachezaji bora zaidi na kutangazwa zaidi na vyombo vya habari, alisema Robin Toskin, mwandishi wa habari wa michezo anayeandikia gazeti ya Standard Group.
"Ubora wa mpira wa miguu ni mkubwa zaidi kwa sababu tuna wachezaji wazuri katika ligi," aliiambia Sabahi.
Mechi za ubora wa juu zaidi na makundi makubwa ya watu pia kumesaidia kuongeza ushindani miongoni mwa timu na wapenzi, alisema.
Miaka kumi iliyopita, timu za AFC Leopards na Gor Mahia zilikuwa hazina ufadhili na mechi zao zingeweza kuvutia watu kidogo si zaidi ya 100, Toskin alisema. Kinyume chake, mechi iliyochezwa na timu hizo mbili tarehe 22 Septemba katika Uwanja wa Kimataifa wa Moi uliwavutia watu 25,000.
Wafadhili sasa wanazivutia familia nzima, kutafutia soko mpira wa miguu kama shughuli ya furaha kwa familia na kutoa burudani katika kabumbu ili kuwavutia vijana, alisema.
Kuna mizunguko minne iliyobakia katika Ligi Kuu na mwisho wa msimu unakaribia kukamilika. Ushindani mkuu ni baina ya timu zinazoongoza sasa za Tusker, AFC Leopards, Gor Mahia na Ulinzi Stars.
"Wakati ligi inakaribia kumalizika, tutashuhudia wapenzi wengi wakimiminikia viwanjani ili kuunga mkono timu zao kwa vile kombe sasa lipo tayari kunyakuliwa," Toskin alisema.

No comments:

Post a Comment