Naendelea kunukuu usemi wa Mwenyekiti wa CCM Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete “Nimebahatika kukaa serikalini muda mrefu hiyo sera ya bure tulijaribu na ikatushinda na wakati huo Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, tulikaa naye tukaona hilo haliwezekani tukaamua tubadilishe sasa nawashangaa wenzetu wanawadanganya eti watatoa Elimu bure.” Mbona nyie wote mlisomeshwa bure mnachopinga ni kitu gani jamani nyie vihiyo wa CCM.
Kwa
upande wake Dk Slaa akiwa mjini Arusha katika moja ya mikutano yake alisema
kwamba CCM walikuwa wakipinga sera ya elimu bure hadi sekondari kutokana na
kulea Wezi, Wabadhirifu na kuthamini anasa kuliko maendeleo kwa wananchi. Leo
hii wameona Watanzania wamejua na kushuhudia wanaibiwa Kodi zao, Madini yao, Wanyama wao, Misitu yao,
Samaki wao, Ardhi yao,
Ndugu Nape Mnauye anataka kudanganya umma wa Watanzania tena wasomi kuliko yeye
kuwa eti “ELIMU BURE” ni sera ya chama chake cha CCM. Hivi huwaga nyie CCM
mnapotoa matamshi yenu huwa hamrudii kuzisoma hotuba zenu mliziwahi kutoa kwa
Watanzania.
CCM
mkitaka msimame kwenye majukwaa hapa Tanzania na watu wawaamini sasa hivi kama
wanavyoweaamini CHADEMA inabidi mrudishe kwanza mali za umma mlizikwiba, fedha
za umma mlizoficha ulaya, mfute mikataba ya hovyo kabisa ya madini mliyowekeana
na wawekezaji, muwatoe Wazungu wote mliowamilikisha ardhi ya Watanzania,
Muwafukuze wawekezaji wote mliowapa vitalu vya kuua na kuuza wanyam wetu, na
mrudishe elimu ya Watanzania iwe sawa kwa wote. Kwa kifupi mkubali kuwa
masikini kama walivyo Watanzania.
Kusema
kweli nyie CCM sasa hivi kushindana na CHADEMA ni ndoto za Alinacha au
Abunuasi. Watanzania hawana imani na nyie tena. Kama
kwenye uchaguzi wenu tu wa chama mnatumia mabilioni kuhonga nani anawaamini
tena kuwakabidhi nchi. Kama mnawavunjia watu
nyumba zao na kuwaacha wanalala nje nani tena ana imani na nyie. Kama mnawauzia hata wagonjwa wa ukimwi dawa bandia nani
ana imani na nyie tena. Kama fedha za misaada
ndizo mnaingiza kwenye uchaguzi na kuzitumia kwa rushwa nani tena anawaamini.
Anayeiamini CCM sasa hivi ana kasoro za akili. Aende akapime Mirembe.
Mwisho
na kila Mtanzania anielewe. CCM wakitaka Watanzania wawaamini warudishe mali zote za
umma wanazomiliki na wahakikishe wanajitoa kwenye biashara wanazofanya na
wawekezaji. Viongozi wa CCM ndio wauza mafuta, Viongozi wa CCM ndio wenye
Mabenki, Viongozi wa CCM ndio wenye mahoteli makubwa makubwa, Viongozi wa CCM
ndio wenye mashamba makubwa makubwa, Viongozi wa CCM ndio wenye mashamba ya
mifugo, Viongozi wa CCM ndio wenye makampuni ya kuagiza magari, Viongozi wa CCM
ndio wenye viwanda vikubwa vikubwa. Viongozi wa CCM ndio waliowadanganya
Watanzania kuwa Serekali haiwezi kufanya biashara ili wafanye wao. Wakadiriki
kuviua viwanda vyote nchini kikiwepo cha Matairi kule Arusha. Mimi nilishangaa.
Magari yalivyo mengi Tanzania
unadiriki kukiua kiwanda uagize tairi Kenya.
Eee
Uwiiiiiii, narudia tena Watanzania Eeeeee Uwiiiiiiii Rushwa, Rushwa, Rushwa
haitatoka Tanzania
bila kukitoa chama tawala cha CCM madarakani. Misaada inakuja toka nje
haiwafikii Watanzania kisa eti wanakiimarisha chama kishinde uchaguzi mwaka
2015. CCM wako madarakani kuhakikisha wanashinda kwenye chaguzi mbalimbali
lakini sio kuhudumia Watanzania. Mimi nawaambia CCM sasa hivi Tanzania hakuna
mjinga. Tena mahali mliharibu kuwekana nyie na wake zenu, na watoto wenu
madarakani. CHADEMA tunawapa kura za “NDIO” mwaka 2015 nchi nzima na zungukeni
kuwaamsha Watanzania wanaosubiri kupata maisha bora wakiwa ndani ya CCM. Msibishane
majukwaani wala bungeni na hawa wajinga tangazeni sera zenu muwakomboe
Watanzania kama alivyofanya Kamanda Robert Mugabe wa Zimbabwe. Ukitegemea kupata maisha
bora ukiwa chini ya utawala wa CCM utasubiri sana.
Mkereketwa
Lengai
Ole Letipipi
No comments:
Post a Comment