Tamasha
la 2 la Jinsia ngazi ya wilaya
-Mkambarani 2012
Mtandao wa Jinsia
Tanzania [TGNP] kwa kushirikiana na Mitandao ya Wanaharakati wa Masuala ya
Jinsia, Haki za Binadamu na Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi wanawaletea
Tamasha la 2 la Jinsia katika ngazi ya Wilaya.
MADA KUU Ya mwaka huu
ni: Haki ya Uchumi: Ni Suala la Kikatiba
, Rasilimali Ziwanufaishe Wanawake Walioko Pembezoni
Tamasha hili
litafanyika Morogoro Vijijini, Mkoa wa Morogoro katika viwanja vya Moseka
vilivyoko Mkambarani nje kidogo ya mji wa Morogoro.
Kuanzia
Tarehe 21-23 Novemba
2012 , SAA 3 ASUBUHI HADI – SAA
10 JIONI
Ushiriki
ni wa wazi kwa watu binafsi, vikundi,
taasisi, mashirika na mitandao mbalimbali.
Unaweza kushiriki kwa njia ya kutoa burudani – ngoma, nyimbo maigizo,
mashairi, visa mkasa, maonesho, kuandika na kuwasilisha mada kwa njia
mbalimbali,kualika na kufadhili ushiriki wa watu wengine.
Kwa
mawasiliano zaidi wasiliana na Waratibu wa Tamasha
Wanawake,
Shika Hatamu , Leta Mabadiliko!
WOTE
MNAKARIBISHWA!
No comments:
Post a Comment