Uharamia
na biashara ya usafirishaji wa binadamu ni changamoto inayotafutiwa
ufumbuzi na vyombo vya Usalama vya Umoja wa Maendeleo wa Nchi za Kusini
mwa Afrika (SADC).
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Arusha leo Mkuu wa kitengo cha Ulinzi na
Usalama cha SADC, Kanali Gerson Sangiza alisema dunia kwa ujumla bado
inaangalia namna ya kutatua tatizo hilo.
Alisema
ufumbuzi wa suala hilo ni mgumu kutokana na ukweli kwamba maharamia
na wale wanaojihusisha na biashara ya uuzaji wa binadamu hushirikiana
kwa karibu na kwa siri na wananchi wa nchi husika. "Tatizo ni kwamba
wananchi ndiyo wanaoendesha vitendo hivyo kwa hiyo namna ya kuwakamata
inakuwa ni shida" Alisema Kanali Sangiza.
Mkuu
huyo aliongeza kuwa ili kukabiliana na tatizo hilo ushirikiano wa
karibu kati ya wananchi na taasisi zinazoshughulikia masuala hayo
unahitajika. Mpaka sasa nia na madhumuni ya biashara hiyo ya uuzaji wa
binadamu bado haijajulikana
na wale waliokamatwa wakijihusisha na bado wanashikiliwa.
"Inasikitisha
kuona binadamu wengi wanasafirishwa kutoka Somalia kupitia Kenya,
Tanzania, Malawi na kupelekwa Afrika ya Kusini ambapo mpaka sasa Afrika
kusini ina wahamiaji haramu milioni tano", alisema kanali Sangiza.
Mkuu
huyo wa kitengo cha Ulinzi na Usalama cha SADC alisema pamoja na tatizo
la uharamia na usafirishaji wa binadamu, nchi wanachama wa Jumuiya hiyo
pia zinakabiliwa na changamoto ya matishio ya kufanyika kwa vitendo vya
kigaidi ambavyo vinahatarisha uhusiano kati ya nchi zilizoendelea na
zile zinazoendelea.
SADC
kupitia chombo chake cha Ulinzi na Usalama imeandaa mikakati maalumu
kuhakikisha kwamba nchi wanachama wa jumuiya hiyo hazisumbuliwi na
matatizo ya uharamia na usafirishaji wa binadamu. Katika hatua ya
kukabiliana na changamoto hizo, wakuu wa Polisi wa nchi zote 15 za SADC
walikutana mwezi Septemba Zanzibar ili kujadili mambo mbalimbali ya
ulinzi na usalama likiwemo tatizo la uharamia na biashara ya
usafirishaji wa binadamu.
No comments:
Post a Comment