THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
Kikwete azindua shule ya kisasa Z’bar
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Jumamosi,
Januari 12, 2013, amezindua shule mpya na ya kisasa kabisa ya Sekondari ya
Mlimani-Matemwe, Mkoa wa Kaskazini Unguja, kwenye pwani ya kaskazini ya
Zanzibar.
Uzinduzi
wa shule hiyo yenye majengo na huduma za kisasa ikiwa ni pamoja na maabara za
masomo ya fikizia, kemia, biolojia na kompyuta ni sehemu ya Sherehe za Miaka 49
ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambayo sherehe zake zimefanyika kwenye Uwanja wa Amaan, mjini Zanzibar, na
kuhudhuriwa na Rais kikwete.
Shule
hiyo iliyogharimu kiasi cha Sh. Bilioni 1.8 mpaka sasa ni moja ya shule 19 za
sekondari zinazojengwa Tanzania Visiwani chini ya Mradi wa Uimarishaji wa Elimu
ya Lazima (ZABEIP) miaka mitano unaogharimiwa kwa pamoja na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar na Benki ya Dunia.
Serikali
ya Mapinduzi (SMZ) inatoa dola za Marekani milioni sita na Benki ya Dunia dola
za Marekani milioni 42 ikiwa ni mkopo wenye masharti nafuu na mradi wenyewe ulianza
kutekelezwa Julai 2008 unafikia mwisho wake Juni mwaka huu, 2013.
Chini
ya mradi huo, zinajengwa shule 10 za sekondari (kidato cha kwanza hadi cha
sita) katika kila wilaya za Tanzania Visiwani, zinajengwa shule tisa za
sekondari (kidato cha kwanza hadi cha nne) – tano Unguja na nne kisiwani Pemba,
kinajengwa chuo kipya cha ualimu cha William Benjamin Mkapa Kisiwani Pemba na
shule sita zinafanyiwa matengenezo makubwa.
Mradi
huo pia ni matokeo ya mazungumzo kati ya Rais Kikwete na uongozi wa Benki ya
Dunia wakati alipofanya ziara yake ya kwanza Marekani mwaka 2006 baada ya kuwa
amekuwa Rais wa Tanzania ambako aliushawishi uongozi wa Benki hiyo kukubali
kutoa fedha za kugharimia mradi huo mkubwa zaidi kuliko mwingine wowote
kufanywa na Serikali katika historia ya Zanzibar.
Aidha,
kutekelezwa kwa mradi huo ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) kwa Uchaguzi Mkuu wa 2010 ambayo iliiagiza Serikali ya
Mapinduzi kujenga shule za kisasa za sekondari 21 katika wilaya zote za Unguja
na Pemba.
Chini
ya Mradi wa ZABEIP, tayari shule za sekondari 13 zimekamilika kujengwa na
ujenzi wa shule sita zilizobakia pamoja na Chuo cha Ualimu cha Benjamin William
Mkapa Kisiwani Pemba unaendelea.
Na
ili kufikisha idadi ya shule 21 za sekondari kama inavyoelekeza Ilani ya CCM,
ujenzi wa shule nyingine mbili zilizosalia unaendelea katika eneo la Mkanyageni
Kisiwani Pemba na Kiblateni Kisiwani Unguja kwa gharama ya pamoja ya Serikali
ya Mapinduzi na Benki ya Kiarabu ya Maendeleo (BADEA).
Shule
ya Mlimani-Matemwe yenye huduma kamili za elimu na ambayo ni sekondari ya
kidato cha kwanza hadi cha nne, ilianza kupokea wanafunzi Septemba mwaka jana
kwa vidato vya kwanza na tatu. Wanafunzi 231 ndiyo walianzisha shule hiyo ya
kutwa na yenye hadhi ya wilaya ikiwa na wavulana 145 na wasichana 86. Shule
hiyo ina walimu tisa wakiwemo wawili wa kujitolea kutoka Nigeria.
Sherehe
hizo za uzinduzi wa shule hiyo zilizohudhuriwa na viongozi wa SMZ akiwamo
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Balozi Seif Idi imehudhuriwa na
mamia ya wakazi wa eneo la Mlimani-Matemwe.
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar
es Salaam.
14
Januari, 2013
No comments:
Post a Comment