Mwigizaji wa Filamu Sajuki amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Muhimbili ambako alikuwa amelazwa baada ya hali yake kubadilika kutokana na maradhi yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu, Sajuki alikuwa amelazwa katika dodi ya Mwaisela akipigania maisha yake katika hospitali hiyo.
Msanii huyo ameugua muda mrefu ambapo aliwahi kwenda India kutibiwa
nchini India na baada ya kurejea kutoka mhuko afya yake iliimarika mpaka alipodondoka jukwaani tena katika tamasha la Bongo Movie jijini Arusha hivi karibuni.
Fullshangweblog imeongea kwa simu na mmoja wa wanafamilia ambaye amesema k
wa sasa shughuli za kuhifadhi mwili wa marehemu Sajuki katika hospitali ya taifa ya Muhimbili zainaendelea na ndugu kadhaa wamekusanyika nyumbani kwake Tabata ambapo taarifa kamili za wapi msiba utakuwa na mazishi zitatolewa baadae.
Chanzo cha habari:Full shangwe
No comments:
Post a Comment