Watu saba wameuawa kwa kupigwa
risasi katika shambulizi karibu na msikiti Kaskazini Mashariki mwa Kenya,
karibu na mpaka na Somalia.
Wanakijiji waliambia BBC kuwa watu
kumi waliokuwa wamejihami waliwashambulia kwa bunduki watu hao wakati walipokuwa
wanaondoka msikitini mapema asubuhi.
Mwanzo wanaume watano waliuawa na
kisha wanawake wawili waliosikia milio ya risasi walipofika kuchunguza, nao pia
wakauawa.
Shambulio linafanyika chini ya wiki
mbili kabla ya uchaguzi kufanyika katika eneo mojawapo ambapo usalama ni tatizo
kubwa.
Wenyeji wa kijiji cha Malaley
wanasema kuwa hakuna kilichoibiwa kwani washambuliaji walitoroka punde baada ya
shambulizi.
Kijiji hicho kiko umbali wa kilomita
45 kutoka kambi ya wakimbizi ya Dadaab ambayo ni makao kwa wakimbizi zaidi ya
laki tano, waliotoroka vita nchini Somalia.
Katika mwaka mmoja uliopita, eneo
hilo limekumbwa na mashambulizi ambayo yamelaumiwa kwa kundi la wapiganaji wa
kiisilamu Al Shabaab.
Al-Shabab iliahidi kulipiza kisasi
wakati wanajeshi wa Kenya walipokwenda Somalia kupambana nao, mwezi Oktoba
mwaka 2011 kama juhudi za kusaidia wanajeshi wa muungano wa Afrika.
Chanzo.BBC
No comments:
Post a Comment