MKALI wa muziki
wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’ amewalalamikia watu
ambao walimuibia simu yake na kuvujisha wimbo wake mpya ambao anatarajia
kuuachia hivi karibuni.
Akielezea jinsi
wimbo huo ulivovuja jijini Dar es Salaam , Diamond alisema nyimbo
zake huwa anazitunza katika simu yake ya mkononi na simu hiyo ilipoibiwa
akasikia kwamba wimbo huo umeshanza kusikika mtaani.
“Wimbo unaitwa
‘Ukimuona’, ni kati ya nyimbo zangu ambazo zimesimama na zenye maneno Fulani ya
kuwashika mashabiki, kiukweli mistari imesimama, naandaa video yake pamoja na
kuvuja nitaitoa hivohivo maana ni bonge la ngoma,” alisema Diamond.
Alisema kazi
hiyo ataiachia wiki ijayo anaomba mashabiki wake wakae mkao wa kula kwani
anaamini mistari ya kazi hiyo imesimama na inaujumbe katika jamii.
Diamond kwasasa
anatamba na kibao chake cha ‘Kesho’ ambacho kimeliteka soko la muziki huo mbali
na kuwa na vibao vingi ambavyo vinafanya vizuri.
No comments:
Post a Comment