Dk
Shein alifika katika bonde hilo, katika siku yake ya pili ya ziara ya kutembea
mikoa mitano ya Zanzibar, kukagua uharibifu wa kilimo cha mpunga ulioathirika
kutokana na ukosefu wa mvua ambao ni matokeo ya mabadiliko ya tabia nchi.
“kilimo
hiki cha kutegemea mvua hakina muamana...si cha kutegemea…mvua haikunyesha kwa
wakati mazao yamevia na hiya ni matokeo ya mabadiliko ya tabia nchi”alisema Dk
Shein.
Kwa
hivyo aliwaambia wananchi hao kuwa Serikali inajua kuwa suluhisho la tatizo
hilo ni kilimo cha umwagiliaji ambapo alisema “bila ya maji hakuna kilimo…bila
ya mbegu bora hakuna kilimo…tunahitaji madawa ya kuulia wadudu, mbolea
matrekta, vifaa vya kisasa vya kuvunia mazao” Dk Shein alieleza na kusisitiza
kuwa hayo ndio mahitaji ya kilimo cha kisasa.
Aliwaeleza
wananchi hao kuwa baadhi ya vifaa hivyo vipo tayati nchini ingawa havitoshelezi
na kubainisha kuwa vifaa hivyo vimeanza kutumika na tayari wananchi wa baadhi
ya maeneo ya mashamba wameshaanza kufaidika navyo kutoka na matokeo mazuri ya
kilimo cha mazao yao.
Dk.
Shein aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali yake imeamua na tumejidhatiti
kukibadili kilimo ndio maana Serikali inagharimia asilimia 75 ya gharama za
mbegu, madawa na mbolea ili kuwapunguzia wakulima mzigo wa gharama za kununulia
vitu hivyo na kueleza kuwa Serikali imeweka lengo kwa awamu ya kwanza
kulibadili eneo la hekta 8,000 kuwa la kilimo cha umwagiliaji.
Dk.
Shein aliwaambia wananchi hao hatua hiyo imelenga kuiwezesha Zanzibar ifikapo
mwaka 2015 kipindi cha ndani ya miaka miwili ijayo kujitosheleze kwa asilimia
50.
Alibainisha
kuwa tatizo kubwa katika eneo bonde la Kizimbani ni maji ambapo Serikali
inaweza kulazimika kuchimba visima ili kutekeleza ombi la wakulima wa bonde
hilo la kutaka eneo lao liwemo katika mpango wa kilimo cha umwagiliaji.
Wakati huo huo Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo
na Maliasili Bwana Affan Said alieleza wananchi wamekuwa wakitumia uzoefu wao
wa asili kutambua vipindi vya mvua na kwamba viashiria/alama wanazozitumia
haziendani tena na wakati sasa ambapo kuna mabadiliko ya tabia nchi.
Tatizo
la kuharibika kwa mazao hasa mpunga aliongeza Katibu Mkuu huyo liko zaidi kisiwani Unguja kuliko
kisiwa cha Pemba lakini jitihada zinafanyika kuwasaidia wakulima waliopatwa na
kadhi hiyo mbegu za muda mfupi ili waweze kuendeleza kilimo hivi sasa.
Awali
Rais wa Zanzibar na Mweneyekiti wa Baraza la Mapinduzi alitembelea kituo cha
kutolea mafunzo ya kilimo maalum cha mbogamboga kinachoendeshwa na Kampuni ya
Ujenzi ya RANS huko Kombeni.
Said Ameir, Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment