BAADA kukaa kimya kwa muda hatimaye wasanii wakali wa mduara nchini offside
trick wamejitokeza na kusema walikuwa
wanaandaa albam yao inayokuja kwa jina la Nipe Nikupe itakayokuwa sokoni
kuanzia sasa.
Wakizungumza na safu hii, kundi hilo
limesema kipindi chote ambacho walikuwa wametoweka sio kwamba walikuwa wamelala
ila waliamua kufuata utaratibu wa jinsi ya kufanikisha albam yao na pia
kuwasoma wapenzi wa muziki nini hasa wanataka ili wafanikishe hilo suala, na
kwa upande mwingine kusoma makosa yao na kurekebesha pale ambapo wanahisi wanahitaji
kuweka sawa.
“Tunajuwa kimya kimekuwa kikubwa na
tunaelewa wapenzi wa mduara na wapenzi wa muziki kwa ujumla wana hamu sana
kujua nini kinaendelea, tungependa kuwapeni habari nzuri kuwa kusubiri kwenu
kumefikia mwisho,”wanasema.
Wanaeleza kuwa waliamua kutafuta njia ya kuwezesha muziki wao
kuvuka mipaka na kufika kila kona ya
ulimwengu ili kuwapa wapenzi wao ladha
tofauti za dunia kuweza kupata nyimbo
kwa urahisi.
Wanasema album hiyo ya
nipe nikupe ambayo imekusanya nyimbo zao zote zilizotamba tayari imeshaingia sokoni na kwenye maduka ya
online ikiwapo iTunes, Amazon Mp3, Spotify na mengineyo.
Kundi hilo linasema mwitikio
wake umekuwa kinyume walivyokuwa wanategemea, kwani walipoamua
kuingia kwenye soko hilo hawakutarajia
mauzo, ilikuwa zaidi ni kutangaza mziki
wao wa kitanzania na kutengeneza jina la Offside Trick duniani.
Aidha, wamewaomba mashabiki wao
kuwaunga mkono kwa kununua kazi zao.
Ladha ya nyimbo ni kama kawaida ile
ile ya mduara ila wamejaribu kupiga hatua moja mbele ili kutowafanya wapenzi
wachoke na kuwafanya kuhisi kuwa hakuna mpya.
Album ya Nipe nikupe ina nyimbo nane ambazo ni Chatu, Nipe Nikupe, Kiwembe Feat H-Baba, Usinipe Feat Baby J, Harusi Helwa Feat Zinho, Talaka Feat Ommy, Nipe Nikupe (remix) na Babu jinga
No comments:
Post a Comment