Na Mwandishi wetu, Sengerema.
Watu wawili wasiojulikana majina yao na walikotoka wamemuua Juliana Masele (55) mkazi wa Kitongoji cha Senta A, katika Kijiji cha Bupandwa, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza.
Watu wawili wasiojulikana majina yao na walikotoka wamemuua Juliana Masele (55) mkazi wa Kitongoji cha Senta A, katika Kijiji cha Bupandwa, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza.
Tukio hilo lilitokea juzi , siku moja baada ya
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo katika Halmashauri ya
Wilaya ya Sengerema sherehe hizo zilifanyika katika kata jirani ya
Bulyaheke
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa uchunguzi wa kubaini waliohusika na mauaji hayo unafanyika.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa uchunguzi wa kubaini waliohusika na mauaji hayo unafanyika.
Mtoto wa marehemu aliyejitambul;isha kwa jina la
Japhet Masele (36) alisema tukio hilo lilitokea wakati mama yake
(Marehemu) akila chakula cha usiku na watoto wake watano ambapo watu
wasiofahamika walivamia nyumbani hapo na kufanya mashambulizi hayo kwa
kutumia mapanga.
Naye Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho,Vicent
Ngidindi alisema tukio hilo lilitokea baada ya watu wasiojulikana
kumvamia nyumbani kwake saa 2:30 usiku wakati akila chakula cha usiku na
watoto wake.
Ngidindi alisema baada ya watu hao kumvamia
walimshambulia kwa kumkata kwa mapanga sehemu za kichwa chake hadi
ubongo kumwagika chini.
Alisema watu hao pia walimkata mkono marehemu na
kuudondosha chini na kwamba jeraha hilo lilisababisha damu nyingi kuvuja
na kusababisha kiofo.
Alisema watu hao walikuwa wamevalia makoti marefu na kufunika nyuso zao mithili ya maninja.
Alisema watu hao walikuwa wamevalia makoti marefu na kufunika nyuso zao mithili ya maninja.
Alisema baada ya kumjeruhi mama yao waliondoka
pasipo kuchukua kitu chochote wala kumdhuru mtu mwingine na kwamba
hakuna taarifa zozote walizoziacha
Chanzo. Gazeti la Mwananchi
Chanzo. Gazeti la Mwananchi
No comments:
Post a Comment