Mchekeshaji maarufu wa runinga nchini Habibu Mrisho aka Sumaku amesema kundi lake la Kashi kash limeamua kufanya ziara katika mikoa mbalimbali ya Tanzania kwa ajili ya kuuza CD zao za vishekesho.
Akizungumza
na blogu hii jijini Dar es Salaam, Sumaku amesema ziara hiyo itaanza rasmi
mwezi huu waApril, ambapo wataanza na mikoa ya Kilimanjaro na Arusha na kwamba mashabiki wa vichekesho katika mikoa hiyo watafadika kwa vile
wanatarajia kuuza CD zao kwa bei ambayo kila mtanzania anaweza kuimudu lengo ni
kuwafurahisha wateja.
Anasema
wameamua kuuza CD zao wenyewe ili waweze kukusanya mapato mazuri
yatakayowasaidia kufikia malengo waliyojiwekea, ya kuboresha kazi zao za
kisanii na maisha kwa ujumla.
Baadhi ya wachekeshaji wa kash kash maarufu kama mizengwe |
“Tumekuwa
tukizunguka sehemu mbalimbali kuuza CD zetu na tunashukuru kwamba mashabiki
wetu wanatupokea vizuri, tunauza wenyewe ili tupate kunufaika,”anasema.
Kundi la
Kashi Kashi likiwa linaongozwa na Sumaku, limekuwa likifanya kazi na runinga ya
ITV, ambapo wamekuwa wakivuma kwa umahiri wao kutunga stori za kuchekesha.
No comments:
Post a Comment