TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday 30 May 2013

Mtoto aliyetumbukia chooni nchini China arejeshwa kwa mamake.

Waokoaji wakivunja bomba la maji taka kumuokoa kichanga huyo.

Mtoto mchanga aliyeokolewa kutoka bomba la kupitishia maji taka nchini China amerejeshwa kwa mama yake baada ya maafisa wa polisi kubaini kuwa kutumbukia  kwake katika bomba hilo ilikuwa bahati mbaya.

Tukio hilo la kuokolewa kwa mtoto mchanga katika jimbo la Pujiang  lilizua shutuma kali kutoka kwa raia wa China na wahisani wengi walijitokeza kumsaidia mtoto huyo wa kiume.
Mtoto huyo tayari amechukuliwa na mama yake kutoka hospitali.

Mwanaume mmoja ameomba uchunguzi wa kubaini kama mtoto huyo ni wake na kusema ikibainika ni hivyo, yuko tayari kujadiliana na mama huyo jinsi ya kumlea.

Polisi wameamua kuwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 22 hatakabiliwa na mashitaka yoyote.

Mtoto aliyeokolewa kutoka kwenye bomba la kupitisha maji taka baada ya kupatiwa huduma ya kwanza.     
Source. Mo Blog

No comments:

Post a Comment