Mwasiti Almas |
MSANII mkali
wa kike wa miondoko ya zuku nchini Mwasiti Almas amesema anajisikia faraja kuwa
ni miongoni mwa wasanii, waliochaguliwa kupigiwa kura katika kategori 5 kwa
ajili ya kugombea tuzo za Kilimanjaro
kwa mwaka 2013.
Katika
majina ya wasanii waliochaguliwa kugombea tuzo hizo, Mwasiti anashika nafasi ya
tatu kwa kuwa na kategori nyingi ambapo anagombea tuzo ya wimbo bora wa mwaka
kupitia wimbo wake wa Mapito.
Aidha,
anagombea tuzo ya msanii bora wa kike, msanii bora wa kike bongo fleva, wimbo
bora wa kushirikiana Mapito na wimbo bora wa zuku.
Akizungumza
na safu hii, alisema tuzo hizo zimempa changamoto kwa kuona kuwa muziki wake
unakubalika. Akaongeza kuwa anamshukuru Mungu kwani kuchaguliwa kwake kugombea
tuzo nyingi imempa faraja ya kuendelea na muziki kwa kujiamini.
Hata hivyo,
wasanii wanaoongoza kwa kugombea tuzo nyingi nafasi ya kwanza inashikwa na Ommy
Dimpozi akigombea kategori 6 na nafasi ya pili inashikwa na Ben paul anagombea
nafasi 5.
Katika hatua
nyingine, msanii huyo alisema anatarajia kutambulisha ngoma yake mpya
itakayotamba kwa jina la Wengine wiki hii yaani (wiki ijayo), ikiwa ni zawadi
kwa mashabiki wanaopenda muziki wake
No comments:
Post a Comment