TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Wednesday 28 August 2013

Idhaa ya Kiswahili ya BBC kuhamishiwa Nairobi

    

Shirika la Habari la Kimataifa la Uingereza (BBC) lina mpango wa kuhamishia kituo chake cha redio ya Kiswahili pamoja na kitengo cha uzalishaji wa maudhui ya mtandao wa BBC Swahili Afrika Mashariki.

Mkurugenzi wa BBC Global News Peter Horrocks anatarajiwa kutembelea Nairobi kuja kutangaza mpango huo wa kuhamishia kitengo hicho Afrika Mashariki pamoja na uamuzi wa kuileta timu nzima ya BBC Swahili karibu zaidi na wasikilizaji wake wa Afrika Mashariki.

Alisema kila wiki kumekuwa na ongezeko la watu milioni 20 wanaosikiliza BBC Swahili na idadi ya watu wanaotembelea mtandao wa Bbcswahili.com wamekuwa wakiongezeka mwaka hadi mwaka hivyo kuhamishia timu hiyo Afrika Mashariki kutakidhi mahitaji ya watu hao.

Baada ya kukamilika mpango huo, utengenezaji wa vipindi vya Kiswahili vya ‘Amka na Bbc’ utahamishiwa Dar es Salaam Tanzania na kipindi cha mchana Dira ya dunia kitakuwa kikiandaliwa Nairobi, Kenya. Na Uandaaji wa habari za mtandao zitakuwa zikifanywa sehemu zote mbili Dar es Salaam na Nairobi.

No comments:

Post a Comment