TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Friday 13 September 2013

Rais Kikwete apokea hati za utambulisho za Balozi mpya wa Italia



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Ijumaa, Septemba 13, 2013 amepokea hati za utambulisho za Balozi mpya wa Italia katika Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Luigi Scotto.

Katika halfa fupi iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais Kikwete ameishukuru Italia kwa misaada ambayo nchi hiyo imekuwa inatoa kuchangia maendeleo ya Tanzania ikiwamo kugharimia ujenzi wa Barabara ya Dar es Salaam Bagamoyo.

Aidha, Rais Kikwete amemtaka Balozi huyo mpya kuisaidia kuyashawishi makampuni zaidi ya italia kuja kuwekeza katika uchumi wa Tanzania. “Tumekuwa na makampuni makubwa ya Italia yaliyopata kuwekeza katika uchumi wa Tanzania ikiwa ni pamoja na Agip na Incar lakini bado tunahitaji uwekezaji zaidi ili tuweze kuimarisha zaidi uchumi wetu,” Rais Kikwete amemwambia Dkt. Scotto.

Naye Balozi huyo mpya amesema kuwa amefurahi sana kuteuliwa kuwa Balozi katika Tanzania. “Ndoto yangu kubwa tokea nikiwa mtoto ilikuwa ni kufanya kazi katika nchi iliyomtoa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere”.
Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU,
DAR ES SALAAM.

13 Septemba, 2013

No comments:

Post a Comment