Akizungumza kutoa elimu kwa baadhi ya wanafunzi wa
shule hiyo, Meneja Mkuu Ukuzaji Amana wa TPB, Paradise Nkini alisema TPB
imeadhimia kutoa elimu kwa wanafunzi hasa kidato cha tano na sita ili
kuwajengea mazoea ya kuanza kujiwekea akiba hali ambayo itawasaidia hapo
baadaye.
Alisema kwa mipango ya sasa TPB itatoa elimu kama
hiyo katika shule za sekondari ya mikoa ya Dar es Salaam na Pwani na
baada ya hapo elimu kama hiyo itaendelea kutolewa mikoa yote. Alisema
elimu hiyo ya kujiwekea akiba kwa wanafunzi inayotolewa na benki hiyo
inatolewa sambamba na huduma ya 'Platinum Account' ambayo ni akaunti
maalumu kwa wanafunzi iliyoandaliwa kumudu mazingira ya mwanafunzi.
"Tumekuja pia kutambulisha akaunti yetu maalumu kwa
wanafunzi ijulikanayo kama Platinum, hii imeandaliwa kwa ajili ya
wanafunzi na imezingatia kipato chao...kwanza inafunguliwa kwa sh. 5,000
tu, haina makato ya kila mwezi na haina gharama za uendeshaji kama
ilivyo kwa akaunti nyingine," alisema Nkini.
Aidha alisema sambamba na elimu inayotolewa kwa
wanafunzi, TPB inatoa zawadi kwa baadhi ya shule zilizofanya vizuri
kitaaluma na kuwazawadia wanafunzi baadhi ya vifaa vinavyowasaidia
katika masomo yao.
"...Tunatoa zawadi kwa baadhi ya shule hasa
zilizofanya vizuri na zile shule ambazo zinahali ngumu za vijijini,
tunatoa zawadi za madaftari, tunatoa kalamu na kuwashirikisha wananfunzi
waweze kuelewa benki yao vizuri," alisema Nkini akizungumza na
wanahabari kwenye viwanja vya shule ya Kibasila.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
No comments:
Post a Comment