TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Saturday 12 October 2013

Mwapachu ataka 2014 utangazwe mwaka wa EAC

By Isaac Mwangi,EANA
Arusha, Oktoba 12, 2013 (EANA) – Katibu Mkuu wa zamani wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Juma Mwapachu amependekeza kwamba mwaka 2014 utangazwe kuwa Mwaka wa Raia wa Afrika Mashariki katika juhudi za kuzihamasisha nchi wananchama kuanza kujiona kuwa ni wana Afrika mashariki.
 Akizungumza katika siku ya kwanza ya Mkutano wa Jukwaa la Katibu Mkuu wa EAC kwa sekta binafsi,asasi za kiraia na wadau wengine mjini Nairobi,Kenya, Mwapachu alimshauri Katibu Mkuu wa sasa wa EAC, Dk Richard Sezibera kutoa pendekezo hilo kwa baraza la mawaziri na kisha katika kikao cha wakuu wa nchi kitakachofanyika mwezi ujao.

 Mwapachu ambaye saa ni Rais wa Chama cha Maendeleo ya Kimataifa alikuwa anawasilisha mada juu ya ‘’ Kuimarisha Mtangamano wa EAC:Jukumu la Raia.’’
 Akichukua mfano kutoka Umoja wa Ulaya (EU) alitoa wito wa kufanyia marekebisho mkataba wa EAC ili kuweza kuanzisha Juhudi za kuwa na Uraia wa Afrika Mashariki.  
 Mkataba wa EU ulifanyiwa marekebisho na mkutano wa Lisbon,ambao ulianza kutumika rasmi Desemba 2009,kutoa uraia kwa raia wa EU. Mwaka 2013, ulitangazwa na EU kuwa Mwaka wa Raia wa Umoja wa Ulaya.
 Tatizo kubwa linaloikabili kanda ya EAC, Mwapachu alisema ni mtazamo wa washirika wakubwa katika mtangamano wakiwemo viongozi wa siasa,vyombo vya habari na asasi za kiraia kushughulikia mambo yanayohusu jumuiya kutoka katika misimamo ya kitaifa.
 ‘’Katika hali kama hiyo upo ukosefu mkubwa wa uelewa juu ya masuala ya kanda kinyume na masuala ya kitaifa na hivyo kuleta matokeo hasa kwa EAC. Kutokana na hali kama hiyo utahamasishaje fikra za uraia mpana katika mtangamano wa jumuiya nje ya semina, mikutano na makongamano?,’’ aliuliza Mwapachu.
 Mapema mkutano huo ulifunguliwa rasmi na Katibu anayeshugulukia Wizara ya Masuala ya Afrika Mashariki, Biashara na Utalii,  Bi Phyllis Kandie, ambaye alisisitiza umuhimu wa kuwa na mikutano kama hiyo mara kwa mara na wadau ili kupata mawazo na maoni yao juu ya hatua mbalimbali za kuendeleza na kuboresha mtangamano.
 Katika hotuba yake Katibu Mkuu wa EAC, Dk Sezibera alitoa changamoto kwa asasi za kiraia na sekta binafsi kuimarisha ushirikiano mipakani na mitandao mbalimbali na mashirika ili kulifikia lengo la kuleta umoja na mafanikio Afrika Mashariki.
 IM/LC/NI

No comments:

Post a Comment