Habari kutoka Sudan zinasema mapigano makali ya
kikabila kati ya makabila mawili kwenye mpaka wa jimbo la Mashariki mwa
Darfur yamesababisha vifo vya zaidi ya watu mia moja katika siku za hivi
karibuni.
Taarifa nyingine zinasema askari wa Chad waliokuwa wakifanya doria na majeshi ya Sudan katika mpaka baina ya nchi hizo mbili ni miongoni mwa waliojeruhiwa.
Umoja wa mataifa umeonya kuwa mapigano hayo ya kikabila baina ya makabila hayo mawili yamesababisha maelfu ya raia kukimbia makazi yao katika eneo hilo.
Chanzo.Bbc Swahili
No comments:
Post a Comment