Na Isaac Mwangi,EANA
Arusha, Novemba 16, 2013 (EANA) -
Mkutano wa pili wa Amani na Usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
unaofanyika Bujumbura, Burundi umebaini kwamba demokrasia ndogo, kiwango
kikubwa cha rushwa, ukosefu wa haki wa kihistoria pamoja na ukiukwaji wa haki
za binadamu, kuwa ni miongoni mwa hatari za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.
Akizungumza katika mkutano huo Mkurugenzi
wa Taasisi ya Amani na Usalama Afrika, Peter Edobu alitoa wito wa kuimarishwa kwa
demokrasia na utawala wa sheria.
Alisema kuwa kanda ya EAC
inakabiliwa na utofauti katika katiba za kitaifa ikiwa ni pamoja na mifumo
dhaifu na inayopingana ya sheria na sera.
Matatizo mengine yanayoikabili kanda
hiyo aliyataja kuwa ni pamoja na kutokuwepo
na umoja katika masuala ya siasa na kukosekana na ukomavu wake katika nchi zote
wananchama wa EAC.
Sambamba na hayo aliongeza kuna kutoheshimu
taaisisi za kisiasa na viongozi wake na pia kuwepo siasa za kikabila na kidini.
Edobu alisema nchi zote wanachama
zimekuwa zikijihusisha na chagauzi ambazo zimetiliwa mashaka.
Mtoaji maoini katika Masuala ya
Kijamii wa Tanzania, Jenerali Ulimwngu alisema kuongezeka kwa vitendo vya kutovumilina
kidini na ubaguzi ni miongoni mwa changamoto za amani na usalama.
Mtaalamu wa Masuala ya Amani na
Usalama wa EAC, Leonard Onyonyi alizitaja changamoto nyingine za ndani kuwa ni
pamoja na ukosefu wa ajira, usalama wa chakula,wizi wa mifugo na
ujambazi,matumizi ya madawa ya kulevya,uharibifu wa mazingira na ukosefu wa
usalama wa taasisi za maji za kikanda.
IM/LC/MM
No comments:
Post a Comment