Bujumbura,
Novemba 15, 2013 (EANA) - Kushirikisha mashirika yasiyo ya kiserikali katika
juhudi za kutafuta suluhisho la miggoro ya kikanda kunaweza kuimarisha majadiliano
na uvumilivu katika kanda ya Afrika Mashariki.
Hayo yalisemwa na
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi, Bernard Busokoza alipokuwa anafungua
mkutano wa pili wa Amani na Usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
unaofanyika mjini Bujumbura, Burundi.
Alisema juhudi
zinazofanywa za kuleta amani mara nyingi hushughulikia sababu za migogoro
husika badala ya vyanzo vyake.
''Ni mara chache sana
kwa wadau kuhusishwa na mara nyingi pia suluhisho la migogoro huwa ni maagizo
kutoka nje na kutumika kwa pande zote zinazohusika,'' alisema.
Busokoza alisema
mkutano huo utasaidia kujenga uwezo wa pamoja wa kutatua migogoro kwa kwa
wajumbe.
''Mkutano huu utatoa
fursa kwa wadau wote wakiwemo wa umma,binafsi, jeshi,polisi na raia kushiriki
kikamilifu katika kujenga uwezo wa kudumu wa kushughulikia masuala ya amani na
usalama katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na nje ya jumuiya hiyo,''
alifafanua.
Akihutubia wajumbe
katika mkutano huo pia, Waziri katika Ofisi ya Rais anayeshughulikia EAC,
Leontine Nzeyimana alisema hatua maalum zinahitajika kubaini na kuzuia vitisho
dhidi ya amani na shughuli za kigaidi.'' Tunahitaji kuimarisha mitandao yetu ya
kiintelejensia ili kukabiliana vitisho hivyo.''
Naye Naibu Katibu
Mkuu wa EAC anayeshughulikia Shirikisho la Kisiasa, Charles Njoroge alitoa wito
kwa wajumbe wa mkutano huo kuleta mapendekezo ya namna kanda hiyo kwa pamaja
itakavyoweza kukabiliana na vitisho vya kutoweka kwa amani na usalama badala ya
kuingia katika migogoro.
Mkutano huo
unahudhuriwa na wajumbe 150 kutoka nchi wanachama wa EAC, ikiwa ni pamoja na
Kenya, Uganda, Tanzania, Burundi na Rwanda. Umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya
Sektretarati ya EAC na Shirika la Misaada la Kimataifa la Ujerumani (GIZ).
IM/lC/MM/NI
No comments:
Post a Comment