Polisi nchini Burundi wanasema zaidi ya mafuvu 40 ya
binadamu yamepatikana katika makao ya raia mmoja wa Italia anayefanya
kazi nchini humo.
Polisi hata hivyo hawajatoa taarifa zaidi na mwandishi wa BBC nchini Burundi anasema watu wana shauku ya kutaka kujua mafuvu hayo yalitoka wapi na yalikua yatumike kivipi.
Kumekuwepo ripoti za sehemu za miili ya binadamu kutumika katika ushirikina hasa katika nchi jirani ya Tanzania,lakini haifahamiki kwanini mafuvu yaliyopatikana hapo awali yalikua yakipelekwa Thailand.
Bw Favaro amekua akiishi nchini Burundi kwa miaka kadhaa.
No comments:
Post a Comment