TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Thursday 21 November 2013

Rufaa ya Babu Seya yatupiliwa mbali TZ

Mahakama, nchini Tanzania imetupilia mbali ombi la kusikilizwa upya kwa kesi dhidi ya muimbaji Nguza Viking, anayejulikana kama Babu Seya pamoja na mwanawe, ambao walihukumiwa maisha jela, kwa kosa la ubakaji.
 Majaji walisema kua kuna thibitisho tosha kuwa wawili hao waliwabaka watoto 10 wa shule ya msingi mwaka 2013.


Katika kesi yao ya kwanza ya rufaa miaka mitatu iliyopita, watoto wengine wawili wa muimbaji huyo,ambao pia walipatikana na hatia ya kosa hilo mwaka 2004, waliachiliwa.

Kesi hiyo imewashtua mashabiki wa Viking katika nchi hiyo iliyo katika kanda nzima ya Afrika Mashariki.

Mwanamuziki huyo mwenye kuimba nyimbo za Rhumba, ambaye ni mzaliwa wa DRC, ameishi Tanzania kwa miaka mingi na kuwa na ufuasi mkubwa huko.

Mwandishi wa BBC Ben Mwang'onda mjini Dar es Salaam anasema kuwa Viking na kijana wake Johnson Nguza ambaye pia ni mwanamuziki, walifika mahakamani kwa uamuzi huo.

Walionekana kuwa watulivu wakati majaji walipotupilia mbali ombi lao kutaka hukumu yao kubatilishwa.

Walihukumiwa kwa kuwabaka wasichana 10 wa shule ya msingi waliokuwa kati ya umri wa miaka sita na nane wote waliokuwa katika shule ya msingi ya Mashujaa mtaani Kinondoni mjini Dar es Salaam.

Wakili wa muimbaji huyo alisema kua muimbaji huyo hana matumaini tena ya kupewa rufaa kwani hili ndio lilikuwa ombi lake la mwisho.
Chanzo.Bbc Swahili

No comments:

Post a Comment