THE
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone:
255-22-2114512, 2116898
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S
OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX
9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefanya uteuzi wa wakuu wa Shirika
la Utafiti wa Maendeleo ya Viwanda (TIRDO), Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi
ya Ngorongoro na Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa.
Katika uteuzi huo, Rais amemteua Prof.
Mkumbukwa Madundo Angelo Mtambo kutoka Chuo Kikuu cha
Kilimo cha Sokoine kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utafiti wa Maendeleo ya Viwanda
(TIRDO).
Rais pia amemteua Bwana Freddy Safiel Manongi
kuwa Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, ambaye hivi sasa ni
kaimu Mkuu wa Chuo cha Wanyamapori cha Mweka na pia amemteua Prof.
Audax
Zephania Philip Mabula kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam kuwa Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa.
Uteuzi huu umeanza rasmi mwishoni mwa
Mwezi Octoba mwaka huu.
Imetolewa na;
Premi
Kibanga,
Mwandishi
wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu - Dar es Salaam.
11 Novemba, 2013
No comments:
Post a Comment