Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini
jioni ya jana, Jumatano, Desemba 18, 2013, kwenda Marekani kufanyiwa uchunguzi wa
afya yake.
Kwa
mujibu taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ratiba ya shughuli za uchunguzi wa afya yake na kwa kutilia maanani siku
za kusafiri kwenda Marekani na kurudi nchini, Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nchini
Alhamisi ya wiki ijayo, Desemba 26, 2013.
No comments:
Post a Comment