TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Hafla ya
kukabidhi Rasimu ya Katiba kwa Mhe. Rais
Tume ya Mabadiliko ya Katiba inapenda kuwafahamisha wananchi na
wadau wengine wote kuwa Hafla ya kukabidhi Rasimu ya Katiba kwa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mhe.
Dkt. Ali
Mohammed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi itafanyika
siku ya Jumatatu, Desemba 30, 2013 katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es
Salaam.
Hafla hiyo pia inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa Serikali,
vyama vya siasa, taasisi za kidini, asasi za kiraia na wananchi wa kawaida.
Taarifa zaidi kuhusu hafla hii zitatolewa baadaye.
No comments:
Post a Comment