Wanawake 12 ambao ni wazazi wa wasichana 21
waliofanyiwa ukeketaji wilayani Same, mkoa wa Kilimanjaro, kaskazini mwa
Tanzania, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Same, wakati
waliposomewa mashitaka yao kwa mara ya kwanza tangu wakamatwe mwishoni
mwa wiki iliyopita.
Miongoni mwa washitakiwa, mmoja alikabiliwa na mashitaka mawili, moja akiwa mzazi wa mmoja wa wasichana waliokeketwa na pia akiwa ngariba.
Kutokana na mila na desturi ya baadhi ya makabila nchini Tanzania, ukeketaji unafanyika japo ni kinyume cha sheria, huku watu wanaokamatwa kuhusika na ukeketaji wakichukuliwa hatua za kisheria.
Kama watapatikana na hatia, wanawake hao wanakabiliwa na kifungo kisichopungua miaka mitano jela au kutozwa faini kubwa.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 30 Desemba 2013, wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.
Chanzo:Bbc Swahili
No comments:
Post a Comment