Na Baraka Kizuguto, Antalya
BAADA ya sare ya 0-0 jana na KS Flamurtari inayoshiriki Ligi Kuu ya Albania jana viwanja vya Side Stars Complex Manavgat, Antalya, Kocha Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm ameusifu ukuta wa timu yake ni imara.
BAADA ya sare ya 0-0 jana na KS Flamurtari inayoshiriki Ligi Kuu ya Albania jana viwanja vya Side Stars Complex Manavgat, Antalya, Kocha Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm ameusifu ukuta wa timu yake ni imara.
Alisema vijana wake wamecheza vizuri mechi ya jana na kwa ujumla timu zote ziliweza kucheza kwa nafasi, lakini kwa umakini wa walinzi wa timu zote ndio maana milango ilikua migumu kufunguka.
Yanga SC jana |
“Washambulaji wetu walipata nafasi kadhaa, lakini hawakuweza kuzitumia vizuri, hali kadhalika mlinda mlango wetu Dida aliweza kuokoa hatari nyingi kipindi cha pili kutoka kwa wapinzani wetu” alisema Hans.
Katika mechi za awali, mabingwa hao wa Tanzania Bara, Yanga walishinda mbili dhidi ya Ankara Sekerspor mabao 3-0 kabla ya kuifunga Altay SK 2-0.
No comments:
Post a Comment