Arsenal imepoteza nafasi ya
kurejea tena kileleni mwa ligi kuu ya Premier, baada ya kutoka sare ya
kutofungana bao lolote na Manchester United katika uwanja wao wa
nyumbani wa Emirates.
Licha ya kuwa mechi hiyo ilikosa ladha ya hadhi ya timu mbili kuu zinapocheza, pande hizo mbili zilipoteza nafasi nyingi za kufunga.
Hata hivyo ilibidi timu hizo mbili kugawana alama moja kila moja na Sasa Arsenal imesalia katika nafasi ya pili na alama 56 alama moja tu nyuma ya Chelsea.
Aliyekuwa mchezaji wa Arsenal Robin Van Persie, nusura aifunge klabu yake ya zamani lakini juhudi zake zilizimwa na Wojciech Szczesny.
Olivier Giroud naye alipoteza nafasi nzuri zaidi ya Arsenal ya kufunga Man United.
Manchester United yasalia nafasi ya saba
Wakati huo huo, hali mbaya ya anga ilisababisha mechi mbili za ligi kuu ya premir kuhairishwa jana usiku.
Mechi kati ya Manchester City na Everton ilihairishwa kutokana na upepo mkali ili hali mjini Everton, Polisi waliwashauri masimamizi wa klabu hiyo kuhairisha mechi yao na Cyrstal Palace kwa sababu jengo moja lililokuwa karibu na uwanja huo uliporomoka.
Chanzo.Bbc Swahili
No comments:
Post a Comment