Klabu ya Arsenal imerejea juu
katika jedwali la ligi kuu ya Premier baada ya ushindi wao wa 2-0 dhidi
ya Crystal Palace katika uwanja wa Emirates.
Oxlade-Chamberlain aliongeza bao la pili kutokana na pasi ya Olivier Giroud.
Matokeo hayo yanaiweka Arsenal kifua mbele kwa alama juu ya Manchester City, ingawa vijana wa Manuel Pellegrini,wanaweza kuchukua nafasi ya kwanza ikiwa watashinda Chelsea katika uwanja wa Etihad katika mechi ya leo.
Lakini Arsenal, wanaojitahidi kupata ushindi wa ligi, walipata pointi tatu na kusonga mbele ya Liverpool kwa pointi tatu.
Wanatarajiwa kumenyana na watani wao Manchester United baadaye.
Chanzo:Bbc Swahili
No comments:
Post a Comment