Meneja
katika Kitengo cha Kitengo cha Bidhaa za Kuwekeza na Wateja Wakubwa,
Dorothea Mabonye akibonyeza kitufe ili kumpata mshindi wa droo kubwa ya
promosheni ya Weka Upewe ya benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Mteja
wa benki hiyo, Mary Malifedha Popote kutoka Kigoma amejishindia gari
jipya aina ya Suzuki Swift lenye thamani ya shs milioni 28. Wengine
kutoka kushoto ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (GBT),
Abdallah Hemedy, Meneja wa NBC Kanda ya Ziwa, Gaudence Shawa na Mkuu wa
Huduma Rejareja za Kibenki wa NBC, Musa Jallow.
Mkuu
wa Huduma Rejareja za Kibenki wa NBC, Musa Jallow (katikati)
akizungumza katika hafla ya droo kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya
NBC jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni, Meneja wa NBC
Kanda ya Ziwa, Gaudence Shawa, Kaimu Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa NBC, Raymond Mutagahywa na Meneja wa Kanda w NBC, Rachel Mwalukasa.
Meneja
wa Kanda wa Benki ya NBC, Rachel Mwalukasa (katikati) akizungumza na
mshindi wa droo kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya benki hiyo jijini
Dar es Salaam leo. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa NBC,
Raymond Mutagahywa na Mkuu wa Kitengo cha Kuwekeza na Wateja Wakubwa,
Andrew Massawe
No comments:
Post a Comment