Seleman Kidunda |
BFT
imechagua wachezajii sita kwa ajili ya kambi ya mazoezi ya Uturuki kwa ajili ya
maandalizi ya michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Glasgow, Scoatland
kuanzia Julai 23-Agosti 3, mwaka huu.
Kati ya
mabondia waliochaguliwa ukimwondoa Nasser Mafuru aliyepata nafasi hiyo wengine
wote ni chipukizi kwasababu hawakuwahi kushiriki mashindano makubwa ya
kimataifa.
Waliotemwa
ni Bondia Seleman Kidunda ambaye aliwahi kushiriki mashindano ya Olimpiki mwaka
2012 London, Uingereza na yale ya Jumuiya ya Madola mwaka 2010.
Wengine ni
Hashim Simon, Joseph Martin, Sunday Elius, Revocatus Omary, Gerald Maechichi na
Haruna Swaga.
Msemaji wa
BFT Salum Viduka ametaja mabondia sita
walioteuliwa katika timu hiyo kuwa ni Hamad Furahisha wa Magereza, Ezra
Paulo wa Kigoma, Mohamed Kidari wa Tanga, Ally Boznia wa Tanga, Mohamed Hakim
wa Kawe na mkongwe mmoja ambaye ni Nasser Mafuru.
“Mabondi hao
na Kocha mmoja Jonas Mwakipesile ndio watakaoenda katika kambi iliyoahidiwa na
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard
Membe, kujiandaa
na mashindano ya Jumuiya ya Madola,”alisema.
Alisema timu
iliyochaguliwa imetokana na mashindano ya kitaifa ya Mandela yaliyofanyika
jijini Dar es Salaam hivi karibuni, na kuongeza kuwa sababu kubwa ya kuwatema
mabondia hao maarufu ni kutokana na kushindwa kushiriki kwenye mashindano hayo
kwa ajili ya kupima uwezo wao.
Viduka
alifafanua kuwa awali, uongozi mpya ulipoingia madarakani uliwaeleza mabondia
wote kurudi katika timu zao, ambapo walitaka washiriki kwenye mashindano ya
Mandela na mabondia wengine wa mikoani ili wapambane na wale wanaofanya vizuri wachaguliwe.
Alisema
matokeo yake mabondia hao maarufu hawakushiriki, ni mmoja tu ndiye
aliyejitokeza na wengine wakidharau.
Kwa mujibu
wa Viduka, mabondia waliochaguliwa kwenda kwenye kambi hiyo ni wachache hivyo
inaweza kuwa vigumu kuleta ushindani na kurudi na ubingwa hivyo wanafanya
mchakato wa kuzungumza na Kamati ya Olimpiki kwa ajili ya kuongeza wengine sita
na makocha wengine wawili.
No comments:
Post a Comment