MKURUGENZI Mkuu wa Kampuni ya usambazaji wa filamu za kiswahili Lufingo Exaud amesema kuwa wameingiza mtaani filamu yao mpya ijulikanayo kwa jina la Xdent ambayo imeshirikisha wasanii mbalimbali wenye majina.
Utakutana na King Majuto, Muhogo
Mchungu, Lufingo, Mzee Pembe na wasanii mbalimbali walio bobea katika
sanaa hii ya filamu nchini.
Filamu hiyo iliyorekodiwa kwa ubora wa
hali ya juu na umakini mkubwa yenye mafundisho ndani yake itakuwa chachu
kwa jamii kujirekerbisha ka.
Kwa sasa filamu hiyo inapatikana maduka yote yanayouza kanda za kiswahili nchini na mikoa yote
hivyo wapenzi wa filamu wanahimizwa kununua
dvd halali ili waendelee kukuza kipato cha wasanii.
Exaud alisema filamu hiyo imekuwa ikigombaniwa sokoni
kutokana na ubora wake pamoja na wasanii wenyewe jinsi walivyo onesha
uwezo mkubwa wa kuitendea haki.
No comments:
Post a Comment