Shirika la Afya duniani WHO limeonya kuhusu kuibuka kwa wimbi baya la maambukizi ya ugonjwa hatari wa saratani kote duniani.
Watu milioni kumi na nne wanajulishwa kuwa wanaugua saratani kila mwaka, lakini idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka na kufikia milioni ishirini na nne katika kipindi cha miongo miwili ijayo.
Taasisi ya utafiti wa kimataifa kuhusu ugonjwa wa Saratani katika shirika la WHO lilionya kuwa gharama ya matimabu inaongezeka kwa kiwango ambacho ni vigumu kumudu.
Taasisi hiyo imesema serikali zinahitajika kutekeleza sheria kali zaidi kuhusu matumizi ya pombe na sukari kama vile kuongeza bei na marufuku ya matangazo ya kibiashara ya bidhaa hizo.
No comments:
Post a Comment