Mwanariadha wa Uingereza Paula Radcliffe analenga kukimbia kwa mara ya mwisho katika mbio za London Marathon za mwaka 2015.
Licha ya Radcliffe, kushinda taji la dunia la Marathon 2005, hajashiriki katika mbio hizo za London tangu 2011 na hajajihusisha na Marathon tangu amalize wa tatu huko Berlin, Septemba, 2011.
Kwa sasa anafanya mazoezi na timu yake ya Uingereza nchini Kenya.
Radcliffe amewahi kushinda mbio za Marathon za New York na amesema kuwa hatastaafu kabla hajashiriki mbio moja ya Marathon.
Mara Yamauchi ambaye ni mwanamke kutoka Uingereza na ana muda bora zaidi baada ya Radcliffe aliiambia BBC Radio 5 live: "Sidhani kama anaweza kurejelea rekodi ya dunia aliyovunja ya 2:15, lakini nadhani anaweza kufikisha 2:20”
Chanzo.Bbc Swahili
No comments:
Post a Comment