Msanii wa
maigizo nchini ‘Dokiii’amesema kwa sasa ameamua kujikita zaidi katika kuimba
muziki wa siasa katika kampeni mbalimbaki
za Chama cha Mapinduzi (CCM) ili kumuunga mkono mama yake ambaye ni
Mwanachama wa Chama hicho.
Akizungumza jana
jijini Dar es Salaam Dokii alisema muziki wa bongo fleva ameuweka pembeni na
kwamba atakuwa akiimba zaidi muziki wa siasa na kuigiza filamu mbalimbali.
“Kwa sasa
nimeweka muziki pembeni unajua tena mama yangu ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya
Taifa(Nec) nimeona nimuunge mkono kuimba
nyimbo za kampeni na zinazohusu CCM,”alisema.
Pamoja na
kuimba nyimbo za siasa alisema nia yake sio kuja kugombea Ubunge baadaye bali
amevutiwa mwenyewe na Chama hicho kwani atakuwa anatumia kipaji chake cha
uimbaji kuelimisha jamii masuala ya siasa.
Alisema pia
pamoja na kuimba muziki wa siasa pia anaendelea na harakati za kuigiza katika
filamu na sasa tayari wameshatoa filamu mbili zinazoitwa ‘sista duu’ na
‘machepele’.
Alisema baada ya siku mbili filamu hizo zitakuwa sokoni hivyo mashabiki wake wasikate tamaa
wataendelea kumuona katika filamu mbalimbali na kuomba wamuunge mkono kwa
kununua kazi hizo.
No comments:
Post a Comment