TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Wednesday 11 April 2012

Mtanzania anayejivunia kupanda vilele saba vya milima duniani

Mtanzania Respicius Baitwa kulia akiwa na Risasi Mwaulanga kushoto wakizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusiana na mafanikio yake ya kupanda vilele saba vya milima duniani huku akiwa amebakiza vitatu ili atimize ndoto zake. Ili aweze kumalizia vilele vilivyobaki ambavyo ni Denali katika bara la Amerika ya Kaskazini, Vinson, Antarctica, Evarest anahitaji dola elfu kumi na sita.
Baitwa ni mwongazi watalii katika mlima wa Kilimanjaro na pia ni Balozi wa Air Tanzania. Alianza safari yake hiyo toka mwaka 2009 na amefanikiwa kuwaongoza watalii 3000 kupitia njia tofauti tofauti za mlima Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment