TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Tuesday 15 May 2012

Filamu ya Bakora sasa yaingia Mtaani


Kikundi  cha Filamu cha Kibaigwa Taijquan kimeachia filamu yake ya nne inayoitwa Bakora chini ya usimamizi mkubwa wa kampuni ya usambazaji ya Splash ambayo iko chini ya Step entertainment.

Akizungumza na gazeti hili Mratibu wa kikundi hicho Yassin Kanyama alieleza kuwa utoaji wa filamu hiyo ulikuwa ni mpango wa mwaka 2012  kwa ajili yakumaliza mkataba wa Splash waliosaini toka mwaka juzi ili kuwa msambazji wao mkuu.

Alisema kwa sasa filamu hiyo tayari imeingia mtaani kwa maana ya sokoni hivyo kwa wale mashabiki wa filamu wanaweza kuipata kwenye maduka mbalimbali ya filamu.
“Tunawaomba mashabiki wetu watuunge mkono kwa nunua filamu zetu kwa vile ndio ajira kubwa tunayoitegemea vijana wengi kwa sasa, kwa kutuunga mkono kutatusaidia kutimiza malengo yetu,”alisema.

Filamu ya kwanza waliitoa mwaka 2010 ilikuwa ikijulikana kama ‘The killing of campsite’ ambayo ilichezwa ikiwa na mtindo wa kareti ambapo walikuwa wakifanya kazi na Zena Video.

Filamu ya pili waliitoa mwaka 2011 ilikuwa ikijulikana kama ‘Kahaba wa mapenzi’ ambapo pia mtindo waliotumia ni ule wa kareti, wakati filamu yao ya tatu inaitwa Jitu na ilifanikiwa kufanya vizuri  na kuwatangaza kwa kiasi kikubwa ambapo ilisambazwa na kampuni ya Splash. 

Kanyama alisema  kwa jinsi ambavyo wanatoa filamu moja ndipo wanapojifunza mambo mengi kwani kila moja hujifunza kulingana na makosa wanayofanya hivyo pia huboresha yale mapungufu ili kutoa filamu ambazo ni nzuri zaidi ya nyingine na kuweza kukubalika katika soko.

No comments:

Post a Comment