Serikali
imesema inatarajia kuanza kulipa fidia ya sh bilioni 2,200,000,000 kwa
wanananchi 1,788 wa Kata ya Mbagala Kuu waliokuwa wamepeleka malalamiko ya
mapunjo ya fidia iliyotolewa kwa mara ya kwanza iliyotokana na mlipuko wa
Mabomu yaliyotokea katika kambi ya Jeshi Mbagala mwaka 2009.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadik alisema jana kuwa baada ya kupokea
malalamiko ya wananchi hao ilifanyika tathmini na ndipo ikapatikana idadi ya
majina hayo.
“Tathmini
iliyofanyika ilikuwa ni kwa wananchi 2132 waliokuwa na madai ya sh biloni
2,236,037,741 na baada ya kupitiwa upya na uhakiki kufanyika jumla ya wananchi
1,788 wamethibitishwa kustahili malipo hayo yenye jumla ya sh bilioni
2,200,000,000” alisema.
Aidha
alisema kuwa timu hiyo ya wataalamu iliyopitia madai hayo ilibaini kuwa madai
ya wananchi 344 waliokuwa na madai yao ya sh 36,037,741 hayakustahili kwa
sababu mbalimbali.
Alisema
kuwa majiya ya watakaolipwa yatabandikwa kwenye mbao za matangazo kwenye ofisi
za mitaa na Kata ya Mbagala Kuu na kwamba zoezi la ulipaji linatarajiwa
kuchukua siku 20-30 na litaanza Juni 25 katika mtaa wa Mbagala Kuu na
litaendelea na mitaa mingine.
Mkuu
huyo alisema kuwa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke
kutoa matangazo kwa njia ya vipaza sauti kwenye maeneo husika ili kuwafahamisha
wananchi juu ya zoezi hilo.
Alisema
kwa kuwa walipaji ni wengi wanakadiria kwamba kila siku watahudumiwa watu 100.
Katika fidia ya awali jumla ya sh bilioni 8 zililipwa kwa wananchi hao ambapo
kwa sasa zitalipwa bilioni 2.2 zitakazofanya fidia hiyo kufikia zaidi ya
bilioni 10.
No comments:
Post a Comment