TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Monday 25 June 2012

Mkazi Dodoma amchinja mke wake


Na. Luppy Kung’alo, Jeshi la Polisi Dodoma.

  Jeshi la Polisi Mkoa Dodoma linamshikilia mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Daniel s/o Lusega miaka (42) kabila mkaguru na mkazi wa Morisheni kata, tarafa na wilaya ya kongwa kwa tuhuma za kumchinja mke wake na kumuua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi Bw. ZELOTHE STEPHEN alisema Tukio hilo limetokea tarehe 25/06/2012 muda (08:00hrs) wa saa mbili asubuhi leo, katika eneo la Morisheni Kata, Tarafa na Wilaya ya Kongwa.

“Mtuhumiwa alikwenda kuripoti mwenyewe katika kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kongwa kuwa amemchinja na kumuua mke wake kwa sababu hamsikilizi.” alieleza Kamanda Zelothe.

Bw, Zelothe alisema mtuhumiwa huyo wakati anaripoti tukio hilo katika kituo cha Polisi alikuwa na barua mkononi ikieleza madai hayo kwa marehemu mke wake, ikiwa na anuani ikielekeza kwa Afisa Usalama wa wilaya ya Kongwa, lakini barua hiyo ameikabidhi katika kituo cha Polisi.

Kamanda ZELOTHE STEPHEN alimtaja mwanamke huyo aliyeuwawa kuwa ni Telophena w/o Machimo umri miaka (34) kabila Mkaguru, muuza mgahawa  na Mkazi wa Morisheni wilayani kongwa

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Bw. ZELOTHE STEPHEN alisema   askari walikwenda kukagua eneo la tukio na kukuta marehemu amechinjwa kwa kukatwa koromeo na akiwa katika dimbwi la damu pamoja na kisu kilichotumika kikiwa kando yake.

Kamanda huyo wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dododma alisema chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi kwa kuwa mtuhumiwa alikuwa akimtuhumu marehemu kwa kutembea nje ya ndoa pia kwa kutoleta matumizi ili hali merehemu ni muuza mgahawa katika eneo hilo

Hata hivyo Kamanda Zelothe alisema mtuhumiwa huyo ana historia ya ugonjwa wa akili kwa mujibu wa maelezo ya wanandugu na viongozi wa kijiji wa eneo hilo.
Mtuhumiwa amekamatwa na anashikiliwa katika kituo cha Polisi Wilayani Kongwa na  atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo mkabili, alisema Bw. Zelothe.

No comments:

Post a Comment