John
Terry, mwenye umri wa miaka 31, na ambaye ni mchezaji soka wa Chelsea na vile
vile timu ya taifa ya England, anashtakiwa kwa madai kwamba alimtukana Anton
Ferdinand, kwa kutumia lugha ya ubaguzi wa rangi katika mechi uwanjani, madai
ambayo John Terry ameyakanusha.
Ikiwa
John Terry atapatikana na hatia, hukumu kali zaidi itakuwa ni kutozwa faini ya
pauni 2,500.
Kesi
hiyo inatazamiwa itaendelea kwa siku tano katika mahakama yaWestminster, mjini
London.
Inadaiwa
kwamba mlinzi huyo waChelsea alimuita mwenzake mweusi, na akitumia maneno pia
yaliyohusishwa na ngono.
Mtaalamu
wa lugha ya kutafsiri yaliyosema kwa kuangalia mdomo, Susan Whitewood, alithibitisha
kwamba matamshi yasiyofaa yalitumiwa na Terry.
kwa hisani ya Mo blog
No comments:
Post a Comment