TANGAZA NASI LEO 0712709630,0756631636 BARUA PEPE gmkojera@gmail.com

Saturday 1 February 2014

CANVAC yazindua kifaa cha utambuzi wa binadamu kwa wale wanaotaka Viza za Canada



KITUO cha maombi ya Visa cha Canada (CANVAC) kimezindua huduma itakayotumia vifaa vya utambuzi wa binadamu (Biometrics) ambavyo vitatumika kwa wale wote watakaokuwa wakiomba visa ya kwenda nchini Canada.

Vifaa hivyo vitatumika  kuchukua alama ya vidole ya mwombaji pamoja na picha zake ambazo zitasajiliwa na kuhifadhiwa mtandaoni.

Kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa kwa vyombo vya habari na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) na kusainiwa na Ofisa wa CANVAC, Katy Kobelski, nchi za Afghanistan, Jamhuri ya Kimemokrasia ya Congo, Eritrea, Namibia, Pakistan, Sudan Kusini na Yemen ndio zitakazoanza kutumia huduma hii.

Taarifa hiyo ilisema kwamba, kwa raia wa Tanzania hawatalazimika kutumia huduma hiyo wakati watakapokuwa wanafanya maombi ya Visa za Canada.

Katy alisema kuwa uanzishwaji wa huduma hiyo hapa nchini  utapunguza upotevu wa muda na gharama ya watu kutakiwa kusafiri kwenda Nairobi kwa ajili ya kuchukuliwa alama za vidole, kwani sasa huduma hiyo itapatikana katika kituo cha CANVAC cha Dar es Salaam.

Novemba 19 mwaka 2013 IOM kwa kushirikiana na ubalozi wa Canada jijini Nairobi, walizindua huduma hiyo nchini Kenya.

Katy alisema faida ya huduma hii ni kwamba inafanyika kwa haraka na itamfanya muoambaji kuweza kupata taarifa zake kwa njia ya barua pepe.

No comments:

Post a Comment